Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Ticker

6/recent/ticker-posts

KULIKONI TENA NDOA YA TIWA SAVAGE NA TEE BILLZ???

upepo mchafu bado umeendelea kuvuruga mahusiano na ndoa za mastaa nyota mbalimbali Duniani kama vile Tyga na Blac Chyna, Future na Ciara na hivi karibuni tumesikia tena Mariah Carey akidai talaka toka kwa mumewe Nick Canon huku kila mmoja akiwa na sababu zake.
kama hiyo haitoshi kwa upande wa Afrika mambo yameonekana kutokuwa mazuri kwenye ndoa mbichi ya hitmaker wa Eminado, mwanadafada Tiwa Savage  kufuatia picha na ujumbe aliopost kupitia ukurasa wake wa Instagram kuashiria kengele ya hatari.
”………. Which means you MrBillz @teebillz323 cannot return me to my parents or exchange me”  aliandika Tiwa na kuambatanisha na picha kama anavyoonekana hapo chini.
Tiwa SavageTiwa Savage alifunga ndoa ya kimila na mumewe ambaye pia ni meneja wake ‘Tee Billz’ mnamo mwezi Novemba mwaka jana na kisha kufwatiwa na bonge la sherehe iliyofanyika  mjini Dubai mwezi Aprili mwaka huu.
Bado haijaweza kufahamika wazi kama wawili hao wameamua kukana kiapo walichokula mbele ya madhabau ya kanisa au la ukizingatia siku za hivi karibu Tiwa amekuwa akionekana akihudhuria peke yake shoo pamoja na matamasha.

Comments