MWANAFUNZI WA KIKE WA SHULE YA MSINGI AKAMATWA AKIBA NDANI YA DALADALA MJINI DSM
Waandishi wa ahabari nao wahakuwa nyuma kufuatilia sakata hilo. |
Maofisa Usalama wakimpeleka mtoto huyo kituo cha Polisi ili kuweza kupata maelezo zaidi na kusubiri wazazi wake waende kumtoa. |
Mwanafunzi huyo wa kike wa Shule ya Msingi Upendo iliyopo Mbezi jijini Dar es Salaam aliyejulakana kwa jina la Irene alipoanza kupekuliwa na maofisa usalama ilionekana mara ya mwisho kuandika ilikuwa ni Aprili 15, 2014 tokea hapo hajaandika, kumbe huwa anawaaga wazazi anakwenda shule huku akiishia Posta jijini Dar es Salaama akilanda landa na mpaka leo alipodakwa.
Katika mahojiano mafupi yaliyofanywa na maofisa hao, ilibainika kuwa mtoto huyo amekuwa na utoro uliokidhiri jambo ambalo hata alipopigiwa mwalimu mkuu wa shule yao ya msingi anaposoma alikiri hilo na kuongeza kuwa mtoto huyo amekuwa akikataa shule kwa muda mrefu pamoja na kupewa taarifa kwa wazazi wao hawakulifuatilia
Comments
Post a Comment